Friday, August 14, 2015

JE,UKO HATARINI?


Joe alikuwa amechoka na kuishiwa na pumzi.  Hata kazi rahisi kabisa kama vile kutembea kuzunguka nyumba au kwenda kwenye gari, ilimfanya apumue kwa shida.  Alikaa ofisini kwa daktari, akiwa amekata tamaa na kufadhaika.  Alikuwa hajapunguza uzito tangu alipokuja miezi miwili iliyopita.  Kufanya mambo yawe mabaya zaidi, alikuwa bado anavuta sigara, na kiwango cha sukari katika damu yake kilikuwa kikubwa.  Lakini alikuwa bado hawezi kuacha kula donati zenye sukari ambazo alikuwa anazila kila asubuhi, akishushia na kahawa yenye sukari au vinywaji vya kola.  Kwa sababu ya kisukari chake namba 2, kuvuta sigara, unene kupita kiasi, na maisha ya kukaa bila kazi za kutumia nguvu, Joe alikuwa ameshikwa na ugonjwa wa moyo miaka miwili kabla, akiwa na miaka 35.  Ulikuja kwa nguvu na kumwacha na kovu kubwa katika msuli wa moyo wake na tatizo la kushindwa kwa moyo kufanya kazi vizuri.

Akiwa na haya kidogo, Joe alielezea wasiwasi wake kwa daktari wake.  “Ndiyo Daktari, nilikuwa najua kuwa hutafurahia kushindwa kwangu kupunguza uzito, na kwa kuwa bado ninavuta sigara kidogo naomba unielewe, sivuti mpaka mapafuni!  Samahani daktari; sipendi kukuangusha.”
Daktari alimtia moyo kwa upole ili azidi kujitahidi, alieleza kuwa kutokana na kasoro ya kusukuma damu iliyotokana na ugonjwa wa moyo, kisukari kisichodhibitiwa, na uvutaji wa sigara, pamoja na uzito wake uliopita kiasi, asipofanya mabadiliko makubwa atakufa akiwa kijana.

Jibu la Joe lilikuwa la ajabu, “Je daktari, inawezekana kubadilishwa moyo?  Nimesikia huwa unabadilishwa.  Je, ninaweza kupata moyo mwingine?”

“Laiti ingekuwa rahisi na sahihi kiasi hicho,” daktari wake alisema.  “Mioyo inayotolewa kwa ajili ya kubadilisha ni adimu sana, na bado kuna kutumia dawa kwa miaka mingi baada ya hapo.  Hiyo ni njia ya mwisho inayoweza kusaidia, lakini inayowezekana kwa watu wachache tu.  Inakupasa kubadili mtindo wa maisha tena mara moja.”  Hatimaye Joe alielewa hatari ya hali yake na kuanza kubadili namna alivyokuwa anaishi.


Mamilioni ya watu huwa wanahangaika na magonjwa yasiyo ya kuambukiza ulimwenguni kote kama Joe:  Magonjwa ya moyo, saratani, magonjwa ya njia ya hewa, na kisukari.  Yote haya yanasababishwa na mambo makuu manne:-  Matumizi ya tumbaku, kutoshughulisha mwili, pombe na vyakula visivyofaa.  Unaweza kuwa hatarini bila kujua.
Share:

No comments:

Post a Comment