Wednesday, December 20, 2017

UMUHIMU WA KITUNGUU SWAUMU NA NYANYA

umuhimu wa kitunguu swaumu

Utafiti wa hivi karibuni umefichua faida ya ndani ya kiafya ya kitunguu swaumu itokanayo na mseto uitwao allicin uliomo katika kitunguu hicho ambao ndio unaokifanya kiwe na ladha na harufu kali ya kunukia.

Wanasayansi waligundua kuwa mseto wa allicin huoza ili kutengeneza sulfenic acid, ambacho ni ki-kemikali kinachochachamaa kupambana na chembechembe za maradhi zinazoweza kusababisha saratani.

Vitunguu maji na vitunguu saumu vina miseto ya chumvichumvi za kioganiki ambayo hujitokeza kusaidia msukumo wa damu na kupunguza mabujabuja ya damu (blood clotting).

Nyanya

Hili ni tunda mashuhuri na lenye virutubisho ambalo kwa kawaida hutumika kama mbogamboga.  Kwa wastani, watu hula takribani kilo 8 za nyanya kwa mwaka.

Nyanya zina aina mbalimbali za viasili vya kurutubisha na visivyorutubisha vinavyohusiana na faida kadha wa kadha za kiafya.

Hii inajumuisha lycopene, vitamin C, A na K, potasiamu, na nyuzinyuzi.

Nyanya moja yenye ukubwa wa wastani inaweza kutoa takribani nusu ya kiasi cha kila siku cha vitamin C anachohitajika kupata mtu.  Viasili mbalimbali vya nyanya vinasadikika kufanya kazi pamoja kuleta manufaa ya kiafya.

Hii ni pamoja na kusaidia kujenga afya ya meno, afya ya mifupa, afya ya ngozi, afya ya nywele, kupunguza shinikizo la damu (BP) na kupunguza viwango vya lehemu pamoja na kupunguza hatari ya ugonjwa wa moyo na saratani.

Baadhi ya vionjo vya nyanya kama vile lycopene hufyonzwa kwa wepesi mwilini pale nyanya zinapochemshwa, iwe kwa kuzipika au kuzichemsha.

Sasa huenda tunazijua faida za kula lishe kamili ya kuleta afya ikiwa ni pamoja na kula matunda na mbogamboga.

Lakini wasichokijua watu wengi ni kwamba juisi ya mbogamboga ndiyo inayosaidia kudumisha urari (Ph) muhimu wa haidrojeni ya mwili.
Share:

No comments:

Post a Comment