Friday, February 3, 2017

MATIBABU YA ASILI YA UGONJWA WA KUVIMBA KWA TEZI YA SHINGO (GOITER)


Kuusafisha mfumo wa damu

Matibabu ya uvimbe wa tezi ya shingo yanapaswa kuanza kwa kuusafisha mfumo wote wa damu na kuanzisha matumizi ya mlo unaostahili pamoja na utulivu na mapumziko ya kutosha.  Kwa kuanzia maji ya matunda kama vile Matufaa maji (Apple), zabibu, mananasi, na machungwa yanapaswa kunywewa kwa mpishano wa masaa mawili na nusu kwa muda wote wa siku kwa siku nne.

Kujiinika

Kujiinika kwa maji ya uvuguvugu kunapaswa kufanywa kila siku kwa kipindi hiki chote ili kusafisha njia ya haja kubwa.

Kutumia Mlo Unaostahili

Baada ya hatua ya kujiinika, mgonjwa anapaswa kuanza kutumia mlo wa maziwa na matunda, akipata milo mitatu kwa siku ya matunda yenye maji kama vile matufaa, mapapai na zabibu yakiwa pamoja na glasi ya maziwa kwa mpishano wa masaa matano.

Mgonjwa anaweza kubadili taratibu mlo wake na kuanza kutumia mlo ulio na virutubisho kamili.  Katika utaratibu huu anapaswa kula matunda yaliyo katika hali ya upya wake (fresh), yasiyo na muda mrefu tangu yachumwe.  Matunda hayo yanapaswa kuwa matufaa (Apples), Machungwa, zabibu, mapeasi, na madalanzi, jamii za karanga zilizo mbichi na glasi ya maziwa yasiyochekechwa kuondolewa mafuta vitumike asubuhi.  Chakula cha mchana kinapaswa kuwa mboga za majani zilizochemshwa au kupikwa bila kuiva, chapati zilizopikwa kwa ngano ya atta isiyokobolewa na glasi ya maziwa mazito yasiyochekechwa mafuta.  Supu ya mboga za majani, saladi za mboga mbichi za majani kama vile nyanya, karoti, letusi, kabeji, celery na tanipu.  Mbegu za Alfalfa, jibini ngumu iliyotengezwa kienyeji na jamii zote za karanga zikiwa katika ubichi zitumike wakati wa usiku.  Glasi ya juisi ya matunda au maziwa inywewe kabla ya kwenda kulala usiku.  Vinywaji kama chai, kahawa, unga uliokobolewa na vyote vinavyotengezwa kwa ngano nyeupe, sukari nyeupe, vyakula vyenye mafuta mengi, nyama yenye mafuta, vyakula vya kiwandani, na achari za kiwandani vinapaswa kuepukwa kabisa na mgonjwa wa uvimbe wa tezi ya shingo.

Mapumziko ya Kutosha

Mgonjwa pia anapaswa kupata muda wa kutosha kupumzika, iwe angalau siku nzima kwa kila wiki kwa miezi miwili ya mwanzoni ya matibabu.

Mazoezi

Pia ni vyema kwa mgonjwa kuanza kufanya mazoezi ya kutosha pale dalili za ugonjwa huu zikianza kupotea.

Mengine ya Kuzingatia:

Madini ya Joto (Iodine)

Vyakula vilivyo na madini joto kwa wingi vinapaswa kutumika bila kipimo kwa muda wote kwani humsaidia mgonjwa kupona haraka.  Vyakula hivi ni pamoja na mboga za majani kama vile Kabeji, vitunguu swaumu, asparagus, oats, karoti, vitunguu na nyanya, strawberries, na mchele usiolowekwa.

Kutumia Maji
Pamoja na hatua hizi, tiba nyingine za kutumia maji zina manufaa katika kuondoa uvimbe.  Hii ni pamoja na kuukanda mwili wote kwa maji kabla ya kwenda kulala na kuukanda mwili wote kwa maji ya baridi unapoamka asubuhi inasaidia pia.  Endapo ukosefu wa choo utakuwa unajitokeza mara kwa mara, hatua zote muhimu zinapaswa kuchukuliwa katika kuliondoa tatizo hilo.

Kuondoa mawazo

Pia mgonjwa anapaswa kujaribu kuliondoa tatizo la msongo wa mawazo na wasiwasi katika maisha yake ya kila siku.  Katika hatua za mwanzoni, kunaweza kuwa na kujirudia kwa dalili za mwanzoni lakini zitakuwa zikijionesha kwa muda mfupi na katika hali isiyo kali sana na kudumu kwa muda mfupi kadri tiba itakavyokuwa inaendelea.  Kikubwa ni kuwa mgonjwa anapaswa kuwa na mtazamo chanya juu ya kupona kwake kwani ndio msingi wa kufanya kazi kwa mafanikio.

Kutokana na yaliyooneshwa hapo juu, utaona kuwa ugonjwa huu unatibika bila shaka yoyote kwa kutumia vitu vya asili kabisa.
Share:

No comments:

Post a Comment