Friday, February 3, 2017

UVIMBE WA TEZI SHINGO (GOITER)

uvimbe wa tezi shingo

Neno Goita ni jina linalotumika katika kuliita tatizo la kuvimba kwa tezi ya thairoidi iliyo katika eneo la shingo.  Kiufasaha, huu ni ugonjwa wa tezi ya thairoidi.  Ugonjwa huu pia unaweza kutokea bila kuonekana uvimbe katika eneo hilo.  Ugonjwa huu unaonekana kuwatokea zaidi wanawake kuliko wanaume, hasa wale wanawake wasiopata muda wa kutosha wa kupumzika na kupata utulivu.

Dalili za Ugonjwa wa Kuvimba Tezi ya Shingo (GOITER)

Dalili za mwanzoni za goita kwa kawaida huwa ni za muda mfupi na hutokea kama mabadiliko madogo ya kihisia na huweza kupitia bila kugundulika.  Baadae mtiririko wa dalili nyingine kama vile huzuni, kupoteza uwezo wa kuzingatia na kulia vinaweza kuonekana vikiambata na kuharibika kwa hisia.  Pia mgonjwa mwenye tatizo hili huwa anakwazika kirahisi sana.

Kunaweza pia kukawa na kuvimba kwa tezi ya shingo lakini hili haliashirii ukubwa wa tatizo kwani hata tatizo linapokuwa kubwa mara nyingine inawezekana usionekane uvimbe ulio wazi.  Dalili hizi huweza kufuatiwa na hisia za uchovu uliopitiliza na kutetemeka kwa mikono pamoja na ukosefu wa nguvu za kuwezesha kutumia misuli ya aina yoyote mwilini.  Kwa baadhi ya wagonjwa macho huweza kutokeza kwa nje.

Kupungua kwa uzito ni kati ya dalili zinazoweza kujitokeza zaidi kwa wale wanaoumwa ugonjwa huu na huweza kudumu mpaka kufikia hatua ambapo mgonjwa anajisikia kuwa mdhaifu kupindukia.

Visababishi vya Ugonjwa wa Kuvimba kwa Tezi ya Shingo

Chanzo kikuu cha kuvimba kwa tezi ni ukosefu wa madini joto katika chakula na kutokea kwa maudhi mengine ya kihisia na kimwili kunaweza kuliongezea tatizo Zaidi.  Chanzo kingine cha kuvimba kwa tezi ya shingo ni pamoja na mazoea ya kula chakula kilichoondolewa uhalisia wake na ambacho hakikupikwa, pia ulaji wa kupita kiasi wa vyakula vilivyopitia kiwandani na vilivyoondolewa ladha asili.

Soma pia MATIBABU YA ASILI YA UGONJWA WA KUVIMBA KWA TEZI YA SHINGO
Share:

No comments:

Post a Comment