Monday, February 19, 2018

KILA RIKA HUPATA UTAPIAMLO


Utapiamlo ni hali ambayo hutokana na kupata chakula ambacho virutubishi vyake havitoshi au viko vingi hadi kusababisha matatizo ya kiafya.

Neno hili hutumika mara kwa mara hasa kurejelea hasa ukosefu wa lishe ambapo hakuna kalori, protini au lishe ya kutosha hata hivyo, hujumuisha pia kupata lishe kupita kiasi (yaani obesity).

Utafiti uliofanyika umeonesha kwamba kulikuwa na watu milioni 925 waliokuwa na utapiamlo duniani miaka saba iliyopita (2010), ongezeko la milioni 80 tangu 1990.

Watu wengine bilioni moja wanakadiriwa kukosa vitamin na madini.  Katika mwaka 2010 utapiamlo wa protini (kwashiorkor) inayoleta nguvu ulikadiriwa kuwa kusababisha vifo 600,000, vilivyo chini kutoka vifo 883,000 katika mwaka wa 1990.

Ukosefu mwingine wa lishe, ambao unaweza kujumuisha ukosefu wa aidini na anemia kutokana na ukosefu wa madini ya aidini na chuma, ulisababisha vifo vingine 84,000.

Ukosefu wa lishe hadi mwaka wa 2010 ulikuwa sababu kwa asilimia 1.4 ya miaka ya maisha kubadilika kwa sababu ya ulemavu.

Takribani theluthi moja ya vifo vya watoto chini ya miaka mitano huaminika kutokana na utapiamlo.  Katika mwaka wa 2010 ilikadiriwa kwamba ilichangia takribani vifo  milioni 1.5 kwa wanawake na watoto, ijapokuwa baadhi ya makadirio ya idadi hiyo huenda yanatakiwa kuwa zaidi ya milioni 3.

Watoto wengine milioni 165 wana matatizo ya kukua kutokana na ugonjwa huu (stanted growth).  Tatizo la ukosefu wa lishe ni wa kawaida sana katika nchi zinazoendelea sababu kuu zikiwa umasikini na ukosefu wa elimu lishe, ikiwamo Tanzania.

Aina za lishe

Aina ya kwanza ni ukosefu wa lishe ya protini inayojega mwili (kwashiorkor) na hutambulika kwa dalili kama za kubadilika kwa rangi ya ngozi na nywele (rangi ya kutu), uchovu wa mara kwa mara, kuharisha, kushindwa kukua au kuongeza uzito, kuvimba kwa kisigino, miguu (yaani edema) na tumbo (ascites) pia kinga dhidi ya magonjwa kushuka.

Vyanzo vya protini ni kama maharage, mayai, maziwa, nyama, samaki pia protini ya kwenye mboga za majani kama vile kabeji, spinachi, uyoga salama na matango.

Aina ya pili ni ukosefu chakula cha kutosha kwa ujumla (marasmus) huambatana na uso mwembamba, mbavu na mabega kuonekana kwa urahisi kwa sababu ya kukonda, kuharisha, ukosefu wa maji mara kwa mara, kuharisha, macho kuingia ndani na ngozi kuwa laini kupita kiasi.

Ukosefu wa kawaida wa lishe ni pamoja na madini, aidini inayopatikana kwenye chumvi na vitamin A kama vile karoti, parachichi, viazi vitamu, samaki, papai na mboga za majani kama vile mchicha.  Wakati wa ujauzito, kwa sababu ya hitaji kuongezeka kwa kiasi kikubwa, ukosefu huo hutokea kwa asilimia kubwa.

Katika baadhi ya nchi zinazoendelea lishe kupita kiasi kwa njia ya unene (obesity) imeanza kutokea katika jamii sawa kama za walio na upungufu wa lishe.

Sababu nyingine za utapiamlo hujumuisha anorexia nervosa (hali ya kukataa kula kwa lengo la kupunguza uzito) na bariatric surgery (kupunguza uzito kwa kupunguza saizi ya tumbo kwa njia ya upasuaji).

Kwa wazee utapiamlo hutokea zaidi kwa sababu ya mambo ya kimwili, kisaikolojia pia kijamii.

Chanzo

Kwa njia ya chakula mwili unapokea virutubishi vya lazima kama vile kalori, protini, mafuta, wanga (kabohidrati), vitamin na madini.  Hivyo uhaba au wingi wa vitu hivi kwa muda fulani unasababisha utapiamlo.

Hivyo, kuna aina mbili za utapiamlo: kukosa kiwango cha kutosha cha chakula na kukosa uwiano wa virutubishi katika chakula (hasa ule wa protini).

Utapiamlo hutokea kama mtu hana chakula cha kutosha, yaani uhaba wa chakula kwa ujumla na kuwa na hali ya njaa ya kudumu (marasmus).

Hutokea kama mtu anakosa sehemu muhimu za vyakula kwa mfano protini, vitamin au minerali hata kama vinginevyo anakula chakula kingi na pia hutokea kama mtu anazoea kushiba vyakula bila kujali uwiano wa virutubishi ndani ya chakula (obesity).

Kukosa lishe ya kutosha hutokana na kukosa chakula kizuri cha kutosha.  Hii hutokana na bei ya juu ya chakula na umaskini.

Kukosa kunyonya maziwa ya matiti mapema kwa kutosha kunaweza kuchangia, pia maradhi ya kuambukiza kama vile homa ya matumbo, nimonia, malaria na ukambi ambao huongeza mahitaji ya lishe.

Ikiwa ukosefu wa lishe utatokea wakati wa ujauzito au kabla ya umri wa miaka miwili huenda ukasababisha matatizo ya kudumu katika ukuaji wa mwili ikiwemo na akili.

Ukosefu mkali wa lishe, unaojulikana kama kukosa chakula (marasmus), unaweza kuwa na dalili ambazo zinajumuisha kimo cha chini; wembamba, viwango vya chini sana vya nguvu, na miguu na tumbo kuvimba.

Watu hawa huumwa na kuwa baridi mara kwa mara.  Dalili za ukosefu wa lishe hutegemea hasa lishe ambayo inasemekana.

Tiba

Juhudi za kuboresha lishe ni kati ya njia nzuri zaidi za kusaidia kukua hasa upande wa watoto.  Kunyonyesha kunaweza kupunguza viwango vya utapiamlo na vifo katika watoto, na juhudi za kukuza tabia hii hupunguza viwango vya utapiamlo hasa kwa watoto.

Katika watoto wadogo kuwapa chakula kwa kuongezea maziwa ya matiti kati ya miezi sita na miaka miwili huboresha matokeo.

Kuna pia ushahidi mzuri unaounga mkono virutubishi vya lishe kadhaa wakati wa ujauzito na kati ya watoto wadogo katika nchi zinazoendelea.  Njia zinazofaa ni kuwapa chakula watu wanachokihitaji sana, kuwasilisha chakula na kutoa pesa ili watu waweze kununua chakula katika masoko yao.

Kwa wale ambao wana utapiamlo mkali unaosababishwa na matatizo mengine ya afya wanapendekezwa kupata matibabu hospitalini.  Mara kwa mara hii huhusisha kudhibiti kiwango cha chini cha sukari kwenye damu, halijoto ya mwili, ukosefu wa maji, na kupata lishe polepole.

Viuavijisumu vya mara kwa mara vinapendekezwa kwa sababu ya hatari ya juu ya maabukizo.

Hatua za muda mrefu zinajumuisha kuboresha kilimo, kupunguza ufukara, kuondoa uchafu katika mazingira, na kuwawezesha wanawake hasa kielimu juu ya suala hili la lishe.
Share:

No comments:

Post a Comment