Monday, May 11, 2015

SOYA NI KINGA NZURI YA KIHARUSI



Maharage ya soya yana protini nyingi zaidi ya nyama na mayai.  Protini ndani ya Soya ni asilimia 36.5, nyama ina asilimia 20 na mayai asilimia 12.  Soya pia ina mafuta, wanga na vitamini B na E.  Madini muhimu kwa afya ya binadamu kama vile chuma, potassium, copper, zinc na manganese nayo yanapatikana katika chakula hiki.  Soya pia ina nyuzinyuzi za chakula pamoja na dawa-lishe kama vile phytoestrogen.

Soya husaidia katika kinga ya ugonjwa wa saratani ya matiti na ile ya tezi dume.  Hurekebisha vichocheo vya jinsi na mzunguko wa hedhi na kupunguza maumivu ya tumbo wakati wa hedhi kwa wanawake.  Hii ni kwa mujibu wa utafiti uliochapishwa mwaka 1994 katika jarida la American Journal of Clinical Nutrition toleo la 60.


Pia huimarisha afya na nguvu za tendo la ndoa kwa jinsi zote, hii ni kutokana na L-arginine inayopatikana ndani ya soya.  Inasaidia mama anayenyonyesha kupata maziwa kwa wingi, kwa vile huchochea uzalishaji wa homoni ya prolactine inayohusika na uzalishaji wa maziwa. Soya pia huimarisha mifupa, afya ya moyo na mishipa ya damu kwa kuzuia ugonjwa wa kusinyaa kwa mishipa ya damu.  Hushusha kiwango cha lehamu mbaya mwilini na kuifanya damu kuwa nyepesi; kwa namna hiyo husaidia kuzuia magonjwa ya shinikizo la damu na kiharusi. 
Share:

No comments:

Post a Comment