Monday, October 5, 2015

MAMBO YANAYOSABABISHA KUENDELEA KUWA NA KITAMBI


Kitambi ni nini?  Haya ni mafuta yaliyozidi kuzunguka eneo la tumbo.  Kinaweza kutokea kwa watoto, vijana na watu wazima hata wazee wa jinsia zote.

Mwili wa binadamu una seli bilioni 50-200 za mafuta zilizogawanyika kwenye mwili wa binadamu.  Kwa wanawake zipo sana maeneo ya matiti, nyonga (hips), kiunoni na kwenye makalio.  Kwa wanaume seli zipo sana kwenye kifua, tumboni na kwenye makalio.

Mafuta ya tumbo yanayofanya kitambi hukusanywa kwa njia kuu mbili, ya kwanza, ni mafuta kutoka kwenye tishu zilizo chini ya ngozi na ya pili ni kutoka kwenye ogani za ndani kama moyo na kongosho.

Sababu kubwa ya kitambi ni kukosekana ulingano wa nguvu (kalori) kama vile mtu kula vyakula vinavyotia nguvu sana kuliko jinsi anavyoweza kutumia na kutoa kama taka mwili.

Sababu zingine ni kuwa na chembe za urithi za unene kutoka kwa wazazi.  Kuna sababu za kimazingira na nyingine zisizojulikana.

Vitu kama kukosa usingizi na sababu nyingine zinachangia kuendelea kuwepo kwa kitambi ambacho kinaweza kuashiria maradhi ya moyo, kisukari na baadhi ya magonjwa ya saratani.

MCHANGANUO WA SABABU 10 ZINAZOFANYA MTU KUENDELA KUWA NA KITAMBI

 1.       Unaanza kuzeeka

Kadri unavyozeeka, mwili wako unabadili jinsi unavyo ongezeka na kupunguza uzito.  Jinsi zote; za kike na kiume, hupatwa na kupungua kwa utendaji wa kimetaboliki, kutia ndani kiasi cha kalori zinazohitajika kwa mwili kufanya kazi kwa ukawaida.

Zaidi ya hayo wanawake hupatwa na kukoma kwa hedhi, ikiwa wanawake wataongezeka uzito, mara nyingi uzito huo huwa kwenye matumbo yao.  “Profesa Michael Jensen wa kliniki ya moyo alisema.  Wakati wa kukoma kwa hedhi, uzalishaji wa homoni za Instrojeni na Projesteroni hupungua.  Wakati huohuo homoni ya testosterone huanza kupungua kidogo kidogo.  Mabadiliko ya homoni hufanya wanawake wengi kuendelea kubeba uzito mwingi kwenye matumbo yao.

2.       Kutofanya mazoezi kwa usahihi

Mazoezi ya kulala chali na kuinua mwili kuanzia kiuno hadi           kichwa (Crunches) sio mazoezi yatakayokusaidia kuondoa             kitambi.  Badala yake fanya mazoezi ya stamina                               yatakayokufanya utumie nyama (muscles) za tumbo, mgongo,         nyonga na sehemu zingine za mwili.  Kufanya mazoezi ya               namna hii kutasaidia kuunguza/kutumia kalori nyingi mwilini         na hivyo kufanya mafuta yaliyo maeneo ya tumbo kutumika           pia.

Mazoezi ya kukaa kwa muda jinsi fulani kama unapiga                   pushap kitaalamu inajulikana kama plunk, ndio mazoezi                 yanayofaa kwa kuwa huhusisha matumizi ya nyama za mikono, miguu na makalio.

Kukimbia kila siku ni mazoezi bora kwa mwili na moyo wako ingawa mazoezi kwa ajili ya moyo wenye afya peke yake hayawezi kusaidia maeneo ya kiunoni kutia ndani kitambi.

“unahitaji kufanya mazoezi ya kuondoa uzito pamoja na ya kuweka moyo wenye afya.”  Anasema Dk. Sangeeta Kashyap wa kliniki ya Cleveland.

“mazoezi ya kutafuta stamina huongeza ukubwa wa nyama za misuli kitu kinachofanya mwili wako kuunguza/kutumia mafuta kwa sana na kuondoa kitambi.”  Anasema Kate Patton, mtaalamu wa lishe wa kliniki ya Cleverland.  Patton anapendekeza dakika 250 za mazoezi ya kawaida au dakika 125 za mazoezi magumu kila wiki.

3.       Una mkazo

Kuwa na majukumu mengi ya kikazi, familia, kulipa gharama za shule na bili mbalimbali kama umeme na maji kunaweza kufanya ugumu katika kupunguza uzito usiotakiwa mwilini, hasa kuanzia umri wa kati.  Homoni ya mkazo iitwayo Cortisol huongeza kiasi cha mafuta kinachochukuliwa mwilini na kutanua seli za mafuta.  Uwepo wa kiwango kikubwa cha homoni hii huhusiana kwa karibu na ongezeko la mafuta mwilini.

4.       Unajinyima usingizi wa kutosha

Kama wewe ni mmoja wa watu wale wanaokosa muda wa kutosha kulala kwa ajili ya mihangaiko ya hapa na pale unapaswa kuongeza muda wako wa kupumzika.  Utafiti uliofanywa kwa miaka 16 kwa wanawake 70,000 ulibaini wanawake waliolala masaa matano au chini ya hapo walitarajiwa kuongezeka kilo 14 kuliko wale waliolala masaa 7.  Wataalamu hushauri watu wazima kulala masaa 7 hadi 8 wakati wa usiku.

5.       Una maradhi

Ikiwa kiwango chako cha homoni ya Testosteroni kiko juu inaweza kuashiria kutokea kwa ugonjwa wa ovary (PCOS) ugonjwa utakaosababisha iwe vigumu kupunguza uzito.  “Ikiwa una umbo la tufaa na uzito uliozidi kiasi, ni busara kumuona daktariDkt. Kashyap anashauri, kwa maana hali hiyo inaongeza hatari ya kupatwa na ugonjwa wa kisukari

6.       Mazoezi unayofanya hayatii changamoto za kutosha katika mwili

Ili kuondoa kitambi cha muda mrefu ni lazima kujidhatiti kwenye mazoezi magumu.  Utafiti uliochapishwa na jarida Medicine  and Science in Sports and Exercise, ulionyesha watu waliofanya mazoezi magumu/mazito waliweza kupunguza kitambi haraka zaidi kuliko waliofanya mazoezi mepesi.  “Ikiwa lengo lako ni kuondoa kitambi kabisa, basi huna budi kuchagua mazoezi kuondoa kitambi” asema Natalie Jill, mtaalamu wa mazoezi kutoka San Diego.

7.       Unakula mafuta yasiyohitajika mwilini

Mwili haumeng’enyi aina zote za mafuta kwa njia ileile.  Utafiti unaonyesha ulaji wa vyakula vyenye mafuta kama nyama na maziwa huongeza mafuta tumboni na kufanya kitambi.  Wakati ulaji wa vyakula vya mafuta kama parachichi, samaki na alizeti huweka mwili katika umbo zuri.  Ingawa kula vyakula vyenye mafuta ya aina yoyote hufanya mwili kuongeza uzito na kusababisha kitambi hivyo ni vizuri kufurahia vyakula hivyo kwa kiasi kama jina la blogi yetu.

8.         Unakula sana vyakula vilivyosindikwa viwandani

Vyakula kama mkate mweupe, chipsi, vinywaji vyenye sukari kama soda, juisi hufanya mwili kutanuka/kunenepa.  Kitambi huambatana na kunenepa/kutanuka kwa mwili, hivyo ulaji wa vyakula vya viwandani utarudisha nyuma jitihada/uwezo wako wa kupambana na kitambi.  Vyakula vya asili kama matunda, mbogamboga na nafaka isiyokobolewa ambavyo ni vya asili huufanya mwili kusinyaa na kusaidia kuzuia kitambi.

9.       Hauna hamasa (motisha)

Ni kweli uko tayari kisawasawa kuondoa kitambi?  “kupunguza na kuondoa kitambi kunahitaji ushirikiano wa vitu mbalimbali, vyakula vyenye kutia nguvu kidogo na vyenye nyuzinyuzi kwa wingi pamoja na vyakula vyenye wanga na sukari kidogo huku ukifanya mazoezi ya kupunguza uzito.”  Dk. Kashyap anasema.  Ikiwa umepania kupunguza/kuondoa kitambi unaweza kufanikiwa.

10.   Una umbo la tufaa


“Ikiwa unene wako upo maeneo ya katikati na maeneo ya hipsi (nyonga) na mapaja basi una umbo la tufaa (apple).  Kwa muundo huu wa mwili ikiwa ni wa kurithi basi kupunguza kitambi, itakuwa ngumu sana,” anasema Dk. Kashyap.
Share:

No comments:

Post a Comment