Friday, October 14, 2016

MASWALI 10 (KUMI) AMBAYO LAZIMA UMUULIZE MTAALAMU WAKO WA MAGONJWA YA AKINAMAMA

maswali ya akinamama

1.       Je, Ninayo Maambukizo Yatokanayo na Ngono?

Ni muhimu kwa mwanajinakolojia kufutilia mbali kitabibu kuwa huna maambukizi yaletwayo na ngono.  Kama ikibidi vipimo zaidi kuondoa “Chlamydia” Kaswende, Kisonono na virusi viletavyo UKIMWI lazima vichukuliwe kama ikithibitika kuwa yako maambukizi yatokanayo na ngono, tiba lazima imjumuishe mwenzi wako ili kuzuia maambukizi yasitokee tena.  Uchunguzi wa kila mwaka wa mwanajinakolojia, kwa wanawake unawapa fursa nzuri kubainisha hali zai dhidi ya virusi viletavyo UKIMWI.


2.       Je, Njia Ninayotumia Kuzuia Mimba Ndiyo Inayonifaa Zaidi?

Utakapomtembelea mwanajinakolojia njia za kuzuia mimba zitachunguzwa.  Baadhi ya wanawake wanapata madhara kwa kutumia njia hizi ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa uzito, kwa njia za kuzuia mimba kwa kutumia homoni, hedhi inayozidi na wakati mwingine inatoka kwa vipindi tofauti, kupoteza ashiki na kutohusika na utumiaji wa kila siku wa kidonge.  Kweli, ni vigumu kutabiri mwitikio wa mtu kwa aina Fulani ya njia ya kuzuia mimba.  Pamoja na hayo ni muhimu kujadili chaguzi zingine zilizopo na ikiwezekana badilisha aina hiyo ikibidi.  Kwa wale ambao wamefikia idadi ya familia wanayohitaji, njia za kudumu za kufunga Mirija ya Mke (BTL) au kumhasi mwanaume inaweza kufikiriwa.

3.       Je, Maambukizi ya Mfumo wa Haja Ndogo Yaani UTI ni Kitu Gani?

UTI ni maambukizi yoyote ya mrija wa kupitisha haja ndogo na kibofu (sehemu ya chini ya mfumo wa haja ndogo) au mfereji wa ureta na figo (sehemu ya juu ya mfumo wa haja ndogo) kwa urahisi ni maambukizo yoyote katika mfumo wa kutengeneza au kutoa haja ndogo mwilini.  Mfumo huu kwa kawaida ni safi kabisa yaani haujatekwa na bacteria au kiini cha maradhi.  Mambo mawili kwa kawaida yanasabisha mwanamke ashambuliwe kwa urahisi na UTI:

1)      Mrija wa kupitishia haja ndogo nje kwenye uke ni mfupi kwa hiyo uchafuzi wowote wa bacteria unaweza ukapata urahisi kufika kwenye kibofu.

2)      Mlango wa mrija wa kupitishia haja ndogo upo karibu na Uke na mlango wa haja kubwa.  Kumbuka kuwa mshipa wa kupitishia haja ndogo ni safi kabisa lakini milango wa uke  na mlango wa haja kubwa haviko safi kabisa kwa sababu vinaficha mamilioni ya bacteria.  Hivyo uchafuzi wa mrija wa kupitishia haja ndogo unafanyika kirahisi.  Dalili za UTI zinajumuisha kwenda haja ndogo mara kwa mara tena inayoambatana na maumivu.  Katika hali mbaya sana wakati maambukizi yamefikia sehemu ya juu ya mfumo wa haja ndogo homa, kutetemeka, na maumivu kwenye ubavu vinaweza vikajionesha kwa wazi.  UTI si maambukizi yanatokana na ngono.  Pamoja na hayo inaweza kuboreshewa mazingira na tendo la ngono kwa sababu ya ongezeko la uwezekano wa kudhuru sehemu inayolinda mrija wa kupitisha mkojo usichafuliwe.

4.       Je, Hedhi Yangu ni ya Kawaida?

Mpangalio wa kutoka damu unatofautiana kulingana na mtu mmoja mmoja.  Lakini muda unapaswa kuwa siku mbili mpaka siku saba.  Kipindi kati ya hedhi na hedhi kiwe kati ya siku 21 na 35.  Muda huu ni kipindi kutoka siku ya kwanza ambayo hedhi inatokea mpaka kwenye siku ya kwanza kwa hedhi inayofuata.  Damu inatakiwa iwe nyeusi kwa rangi na haitakiwi kuganda.  Wanawake wengi wana vipindi vya kawaida vya hedhi yao.  Tofauti yoyote kutoka katika mpangilio huu wa kawaida unahitaji uchunguzi na mwanajinakolojia.

5.       Nifanye Nini na Upotevu wa Ashiki?

Wanawake wengi hawako tayari kueleza uzoefu wa matatizo yao ya kingono.  Mengi ya matatizo haya yanaweza yakatatuliwa na mwanajinakolojia.  Kisababishi kikubwa cha ashiki ndogo kwa wanawake vijana ni madawa, hasa hasa yanayoongeza nguvu na vidonge vya kuzuia hofu.  Wanawake wengine wanaeleza juu ya kupungua kwa ashiki kutokana na aina ya njia wanayotumia kuzuia mimba.  Muunganiko wa vidonge vya kumeza kuzuia mimba, homoni ya kike inayoweza kuingizwa kwa sindano au kupandikiza.  Usumbufu au maumivu wakati wa ngono yanaweza kusababisha matatizo ya ngono na sababu kuu inaweza ikawa kutoka matatizo makubwa ya kiutabibu kama maradhi ya uvimbe kwenye mfuko wa uzazi, kuvimba kwa mfupa wa nyonga kwa hali rahisi.  Kama uchachu wa uke na kubadilika badilika kwa ute wa uke.  

Mwanajinakolojia wako anaweza akaanzisha njia za kukupeleka kwa mtaalamu wa tiba ya ngono.

6.       Je, Historia ya Unyanyasaji Kingono au Vinginevyo Ina Madhara Kwenye Afya ya Uzazi Wangu?

Unyanyasaji wa ngono katika watoto na vijana wakubwa inaendelea kutokea katika nchi ya Kenya na nchi zingine.  Utafiti unaonesha kwa ndugu wa karibu huwa ndio wahusika wa makosa haya; Yanaweza kuwepo makovu ya kudumu ya kimwili kutokana na matukio haya lakini mengi zaidi ni yale yaliyo matokeo ya kisaikolojia yaliyijificha na ambayo yanaweza yakajionesha yenyewe baadaye kama magonjwa ya kimwili.  Mtendewa anaelekea kushikilia wasi wasi na mfadhaiko juu ya jambo hilo, halafu anakuza dalili za kimwili mara nyingi maumivu kwenye fupa la nyonga ambayo inaaksi maumivu ya kiakili; kutaja kiwewe cha ngono ya huko nyuma linaweza kuwa la msaada sana kwa mwanajinakolojia kutambua wa ugonjwa huo.  Kama hakuna kinachotajwa mwanamke anaweza akapitia vipimo vingi vikionesha matokeo ya kawaida.  Lakini kama tabibu anajua juu ya mashambulizi ya huko nyuma anaweza kumshauri mhusika moja kwa moja au kumpeleka kwa mtaalamu wa magonjwa ya mawazo na wakati huo huo kuzuia vipimo vingine kuchukuliwa.

7.       Je, Uvutaji Sigara na Utumiaji Kilevi Unaathiri Afya ya Uzazi Wangu?

Uvutaji sigara ni jambo hatarishi kwa kusababisha saratani kwa wanaume na wanawake.  Uvutaji wakati wa ujauzito husababisha kujifungua kabla ya wakati, kujifungua mtoto mwenye uzito wa chini, na kupasuka kwa utando kabla ya wakati wake; kuharibika mimba na hata kifo papo hapo baada ya kuzaliwa mtoto.  Matumizi ya vidonge vya kuzuia mimba na uvutaji  vinaongeza hatari ya ugonjwa wa moyo na kiharusi.  Wanawake ambao wanavuta na kuchelewesha kuzaa mtoto wanajiweka mahali pa hatari kwa ugumba baadaye zaidi kuliko wale ambao hawavuti.  Wanawake wanaovuta wana uwezekano wa kukatika hedhi mapema zaidi ya wale ambao hawavuti.  Unywaji kilevi kwa wingi unavuruga ukuaji na maendeleo wakati wa kubalehe.  Inavuruga mzunguko wa hedhi na utendaji wa via vya uzazi.  Unywaji wa kilevi unaweza ukasababisha ugumba na uharibikaji mimba wa mara moja na pia ukuaji usio wa kawaida wa mtoto na maendeleo yake.

8.       Ni Mara Ngapi Lazima Nifanye Nipime Saratani ya Shingo ya Kizazi?

Saratani ya shingo ya uzazi ni ya pili katika kusababisha vifo vya akina mama baada ya saratani ya matiti.  Lakini inaweza ikazuiliwa kwa kutambua na kutibu mapema kabla ya kujitokeza vitu visivyo vya kawaida vya saratani.  Kwa kawaida wanawake wote walio katika kundi la uzaaji na ambao wamepata uzoefu wa ngono lazima wapime kila mwaka.  Lakini kama kipimo kimefanyika miaka mitatu mfululizo na hali iko kama kawaida basi inaweza ikarudiwa ndani ya miaka mitatu baada ya pale.  Ni wanawake tu ambao wameondoa mji wa uzazi, kwa sababu ambazo hazihusiani na saratani ya shingo ya uzazi, ndio hawana haja ya kupima.

9.       Ni Kitu Gani Kinachosababisha Saratani ya Shingo ya Uzazi na Je Kuna Chanjo ya Kuizuia?

Sasa inafahamika kuwa saratani ya shingo ya uzazi kwa kawaida inasababishwa na “Human Papilloma Virus” (HPV) kirusi cha uvimbe wa mwanadamu.  HPV ni kirusi cha kawaida.  Katika aina nyingi na mbalimbali za HPV baadhi hazina madhara na nyingine zinaweza kusababisha maradhi ya viungo vya uzazi.  Wakati watu wengi wanakisafisha kirusi wale ambao hawafanyi hivyo wanaweza wakapata saratani ya shingo ya uzazi, vidonda kabla ya saratani, na sugu kwenye viungo vya uzazi.  Hivi karibuni chanjo yenye uwezo wa kuzuia saratani ya shingo ya uzazi kwa kuzuia maambukizi ya HPV zimeshaanzishwa.  Moja ya chanjo hiyo inayoitwa “GARDASILTM” (aina za 6, 11, 16, 18).  Mchanganyiko wa chanjo uliokuzwa na MSD nyingine inayoitwa “CERVARIXTM” (HPV 16 na 18) zilizo kuzwa na GSK.  Zipo aina zaidi za mia moja ya virusi hivi vya HPV.  Chanjo za HPV hazitakinga dhidi ya aina zote isipokuwa aina ya 6, 11, 16 na 18 zimechaguliwa kwa sababu zinasababisha zaidi ya asilimia 70 ya saratani ya shingo ya uzazi na asilimia 90 ya sugu kwenye viungo vya uzazi ulimwenguni kote.  Chanjo inaweza isimlinde kwa ukamilifu kila mmoja anayeipata na hivyo ni muhimu kuendelea na vipimo vya saratani ya shingo ya kizazi.

10.   Ni Mara Ngapi Ninapaswa Kufanyiwa Uchunguzi wa Matiti?

Uchunguzi wa matiti ni muhimu katika kutambua uvimbe ambao unaweza ukawa saratani.  Saratani ya matiti ndio sababu inayoongoza kwenye vifo vya wanawake ulimwenguni kote.  Inabidi kila mmoja afanye uchunguzi binafsi wa matiti angalau mara moja kwa kila miezi mitatu.  Kwa nyongeza, lazima uwe na uchunguzi wa matiti ambao unafanywa na daktari mara moja kwa mwaka.  Hii ni lazima ili kutambua utofauti wowote ambao haukutambuliwa na mtu binafsi.  Inapendekezwa kuwa wanawake wenye zaidi ya miaka 40 lazima wafanyiwe uchunguzi wa matiti kwa kutumia eksirei kila mwaka. 
Share:

No comments:

Post a Comment