Thursday, November 24, 2016

HUITENDEI HAKI AFYA YA MWILI WAKO USIPOKULA ASALI

faida za kula asali

Asali ni chakula muhimu ambacho kwa muda mrefu kimekuwa kikisaidia kuongeza ladha ya mlo.  Wapo wanaoitumia kwenye chai, maziwa au kahawa wengine wakiipaka kwenye mkate na baadhi wakiweka kwenye uji wa mtoto au juisi ya familia.

Kwa mujibu wa tafiti za dawa lishe matumizi ya kila siku ya asali yanapunguza kiwango cha lehemu mwilini huku ikisaidia kupambana na magonjwa yatokanayo na uzee.

Waaustralia na Wajapan wanasema asali ina uwezo wa kumpa nafuu mgonjwa wa saratani.  Licha ya faida hizi chache bado asali hufanya kazi nyingi mwilini ikiwamo kuimarisha kinga za mwili.


Asali, ikipakwa sehemu husika, ina uwezo wa kulainisha jipu na kuondoa usaha.  Vilevile, hutuliza maumivu ya tumbo na kurahisisha umeng’enyaji wa chakula huku ikisaidia kutibu vidonda hasa vitokanavyo na majeraha ya moto.

Asali ni msaada kwa wenye matatizo ya kifua na mapafu.  Asali inazuia ugumba na inaamsha hisia za kufanya mapenzi.  Wataalamu wanashauri wapenzi kunywa walau vijiko viwili vya asali kila siku kabla ya kulala usiku ili kuimarisha uwezo wao wa kushiriki tendo.  Asali kutibu mafua.  Wataalamu mbalimbali wa tiba mbadala wanasema kuilamba yenyewe au ikichanganywa na baadhi ya vitu vingine huwa ni tiba tosha ya mafua.

Mchanganyiko wa kijiko kimoja cha asali, mdalasini kwenye kikombe kimoja cha maji ya uvuguvugu unasaidia kuondoa chafya na uvimbe wa koo pia.

Asali ni tiba kwa ngozi ya uso na huwasaidia wenye vidonda vya tumbo.  Hutibu maumivu ya jino, maambukizi ya kibofu cha mkojo, fangasi za miguu na upungufu wa nguvu za kiume.

Hupunguza uzito pia.  Sukari ya asili iliyomo kwenye asali huondoa uchovu hasa kwa wazee.

Wanasayansi wa Chuo Kikuu cha Tiba cha Washington, Marekani wanaeleza sumu ya nyuki inaponya maradhi mbalimbali ikiwamo kupunguza nguvu ya virusi vya Ukimwi bila kuharibu seli za mwili.  Wanasayansi hao wanaeleza sumu hiyo iitwayo melitin iliyomo kwenye mwiba wa nyuki ina uwezo wa kuingia ndani ya mfuko unaozunguka kinga ya mwili wa binadamu na kufubaza virusi vya Ukimwi.
Share:

No comments:

Post a Comment