Friday, February 17, 2017

TIBA YA MSUKUMO MKUBWA WA DAMU




Endapo umeanza kuhisi dalili za kuwa na tatizo hili au umepimwa na kukutwa na tatizo hili likiwa katika hatua za mwanzo, ni rahisi kulitibu endapo utafuata maelekezo yaliyo hapo chini.
Lakini kabla ya kuanza kufuata maelekezo hayo, ni vyema kupata ushauri wa daktari wako kwanza juu ya uwezo wa mwili wako kustahimili tiba za mbadala na kama utatakiwa kutumia dawa za hospitali ni vyema kumaliza tiba za hospitali kwanza kabla ya kuanza tiba hii.  Lakini njia hizi zinafaa hata kwa wale wanaohitaji kuzuia uwezekano wa wao kulipata tatizo hili kwa siku za usoni hata kama hawana tatizo hilo:
1.       Fanya mazoezi ya nguvu:  Njia hii huweza kupunguza kiwango cha mafuta kwenye moyo na mishipa ya damu hivyo huweza kusaidia kuepukana na matatizo ya kupatwa na shinikizo kubwa la damu mwilini.
2.       Epuka matumizi ya chumvi:  Ni ukweli usiopingika kuwa chumvi huongeza madini ya joto mwilini na kuleta ladha kwenye chakula lakini inapaswa kupunguzwa kwani pia inaweza kupelekea madhara ya kupatwa na shinikizo kubwa la damu ikiwa itazidishwa.  Inashauriwa kutotumia chumvi mbichi kwenye chakula.
3.       Kunywa pombe kiasi na ikiwezekana acha kabisa:  Ulevi uliokithiri huleta matatizo mengi kwenye afya ya mwanadamu ikiwemo mapigo ya moyo kwenda mbio na kuchochea ugonjwa wa shinikizo kubwa la damu mwilini hivyo ni vema kuepukana na ulevi uliokithiri.
4.       Fanya kazi za nguvu:  Kitendo cha kukaa kwenye ofisi kwa muda wa masaa 41 kwa wiki bila kutoka jasho kinaweza kukuweka kwenye hatari ya kupatwa na msukumo mkubwa wa damu hivyo ni vema wakati mwingine kufanya kazi za nguvu ili kujiweka fiti dhidi ya maradhi kama haya.
5.       Jiburudishe na muziki:  Wakati mwingine msongo wa mawazo hupelekea matatizo ya shinikizo la damu hivyo ni vema kuiburudisha akili yako na aina ya miziki unayoipenda ili kuondoa mawazo yanayosumbua akili yako.  Kwa kufanya hivi unaweza kupunguza shinikizo kubwa la damu.
6.       Jenga utaratibu wa kutembea kwa miguu:  Kwa kawaida utembeaji kwa miguu husaidia kupunguza tatizo la shinikizo kubwa la damu kwa mwanadamu.  Inashauriwa walau kutembea mwendo wa nusu saa kwa siku ili kuufanya moyo wako upate hewa ya kutosha kusukuma damu vizuri.  Jaribu kuongeza kiwango cha kutembea kadri siku zinavyozidi kwenda.
7.       Anza kutumia viazi:  Matumizi ya viazi, matunda na mboga zenye kiwango kikubwa cha potasiamu vinaweza kusaidia kupunguza tatizo la shinikizo kubwa la damu mwilini.  Tumia potasiamu kwa kiwango cha miligramu 2,000 mpaka 4,000 kwa siku.  Madini haya unaweza kuyapata kwa kula vyakula kama viazi vitamu, nyanya, juisi ya machungwa, ndizi, maharage.
8.       Tumia chocolate nyeusi:  Tafiti zinaonesha kuwa matumizi ya chocolate nyeusi husababisha mishipa ya damu kuwa minyumbufu na kusaidia kupunguza kiwango cha msukumo mkubwa wa damu mwilini.    
Share:

No comments:

Post a Comment