Wednesday, December 20, 2017

MAYAI HUMUEPUSHA MTOTO NA UTAPIAMLO


Ulaji wa yai kwa siku unaweza kuwasaidia watoto wadogo wenye utapiamlo na kuongeza urefu hii ni kwa mujibu wa utafiti wa miezi sita huko Ecuador.

Haijalishi yai hilo ni la kukaangwa au la kuchemshwa bali watafiti wanasema yai ni njia isiyo ghali ya kuzuia udumavu kwa watoto.
Miaka miwili ya kwanza maishani ni ya muhimu sana kwa ukuaji na maendeleo hivyo kudumaa kunaweza kuleta madhara makubwa kwa watoto.

Lishe duni ni sababu kubwa ya kudumaa, pamoja na maambukizi ya utotoni na magonjwa mbalimbali.

Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani, WHO, watoto milioni 155 chini ya umri wa miaka mitano wamedumaa.


Wengi wao wanaishi nchi zilizo na kipato cha chini na cha kati na wataalam wa afya wamekuwa wakitafuta njia za kukabiliana na tatizo hilo.
Share:

No comments:

Post a Comment