Monday, February 12, 2018

KOROSHO HUSAIDIA KUPUNGUZA UNENE


Utafiti uliofanywa kuhusu korosho, umeonesha zina faida nyingi kiafya ikiwamo tiba ya maradhi ya moyo.

Tunaelezwa ulaji wa korosho mara kwa mara husaidia kuweka sawa afya ya moyo kwa sababu licha ya kuwa na kiwango kidogo cha mafuta (fat), lakini pia zina aina ya mafuta (Monounsaturated fats) ambayo hutoa kinga kwenye moyo, aina ambayo huweza pia kupatikana kwenye Olive oil.

Utafiti unaonesha ndani ya Korosho kuna kirutubisho aina ya Oleic Acid ambacho huimarisha afya njema ya moyo na huwafaa hata wagonjwa wa kisukari.

Pia, utafiti uliochapishwa kwenye jarida la masuala ya virutubisho nchini Uingereza (British Journal of Nutrition), ulionesha watu waliopendelea kula korosho na bidhaa zake, kama butter, idadi ya vifo vitokanavyo na ugonjwa wa moyo vilipungua kati asilimia 11 na 19.

Hata hivyo, utafiti huo umebainisha watu wanaotumia korosho angalau mara nne kwa wiki, wameonesha kuondokewa na hatari ya kupatwa na ugonjwa wa moyo kwa asilimia 37, lakini iwapo mtu atakula sana korosho, atakuwa kwenye nafasi nzuri ya kuepuka kushambuliwa na magonjwa.

Korosho ni chanzo kizuri cha madini aina ya Copper ambayo ni muhimu mwilini, lakini pia ina madini yanayoimarisha kinga ya mwili na mifupa na hutatua tatizo la upungufu wa uzalishaji wa nguvu za kiume mwilini.

Faida nyingine kwa watu wanaotaka kupungua mwili, ulaji wa korosho mara mbili kwa wiki husaidia kupunguza uzito uliopitiliza, licha ya kuwa na mafuta mengi pia ni chanzo kizuri cha madini ya kopa, magnesium na Phosphorus.
Share:

No comments:

Post a Comment