Thursday, February 16, 2017

DALILI ZA UGONJWA WA SARATANI


dalili za ugonjwa wa saratani


Kumekuwa na ugumu kwa kiasi kikubwa kwa mgonjwa wa saratani kubaini dalili zake na hii ni kutokana na ukweli kwamba kujitokeza kwa dalili hizo hutegemea zaidi eneo lililoathirika.  Ni vigumu kugundua dalili zake pindi ugonjwa unapokuwa kwenye hatua za awali mpaka pale tatizo linapoanza kuwa kubwa.
Ugonjwa huu humuingia mwanadamu taratibu na wengi wamekuwa hawafahamu viashiria vya mwanzoni kutokana na aina yenyewe ya ugonjwa kutojulikana kwa kina na wahusika.  Miongoni mwa viashiria muhimu vya ugonjwa wa saratani pindi unapoingia kwenye mwili wa mwanadamu ni kama vifuatavyo:
Madhara madogo madogo
Kuna baadhi ya dalili ambazo hujitokeza kwa mgonjwa wa saratani kutegemeana na ukubwa wa tatizo la mhusika.  Mfano saratani ya mapafu huambatana na dalili za kukohoa, kifua kubana.  Mgonjwa wa saratani huanza kusikia maumivu makali pindi saratani inapokuwa imekomaa lakini katika hatua za awali maumivu huwa hayajitokezi.
Dalili za kimfumo
Hizi ni dalili za moja kwa moja ambazo huweza kujitokeza katika mwili wa mgonjwa husika wa saratani.  Mfano uzito kupungua, homa, uchovu wa mara kwa mara, mabadiliko ya rangi ya ngozi, kibofu kushindwa kufanya kazi kwa ufasaha.
Dalili za Metastasis
Hatua hujitokeza pindi ugonjwa wa saratani unapoanza kusambaa katika maeneo mengine ya mwili wa mhusika.  Mabadiliko ambayo yanaweza kujitokeza katika hatua hii ni pamoja na maumivu au kuvunjika kwa baadhi ya mifupa.
Kwa kiasi kikubwa ugonjwa wa saratani unatokana na sababu za kimazingira huku asilimia 5 – 10 ikitokana na matatizo ya vinasaba.
Ni vigumu kuthibitisha moja kwa moja chanzo halisi cha ugonjwa wa saratani kwa mhusika kwani kuna sababu nyingi zinazopelekea athari hizo.  Kwa mfano saratani ya mapafu inahusishwa moja kwa moja na matumizi ya tumbaku lakini bado kuna watu wanapatwa na tatizo hili pasipo kutumia tumbaku.
Ugonjwa wa saratani umegawanyika kutokana na athari zake kwenye seli za mwili wa mhusika kama ifuatavyo:
Carcinoma:  aina hii ya ugonjwa wa saratani huwakuta watu wenye umri mkubwa na mara nyingi athari zake huonekana kwenye maziwa, mapafu, utumbo n.k
Saacroma:  aina hii ya ugonjwa wa saratani hujitokeza kwenye maungo ya mwili wa mwanadamu mfano katika mifupa.
Lymphoma na leukemia:  haya ni matabaka mawili ya ugonjwa wa saratani na athari zake huonekana kwenye mfumo wa damu na mara nyingi huwakuta watoto.
Germ cell tumor:  aina hii ya saratani huathiri moja kwa moja mfumo wa uzazi.
Blastoma:  saratani hii pia huwakumba watoto wadogo kuliko watu wazima.  
Ugonjwa wa saratani kwa kiasi kikubwa unaweza kuzuilika ikiwa visababishi vyake vitakabiliwa ipasavyo na wanadamu.  Asilimia 30 ya vifo vya saratani ambavyo vimetokea kulikuwa na uwezekano wa kuvizuia visitokee kwa kuzingatia masuala yafutayo:

·
        
Kuepuka matumizi ya tumbaku, ugoro na mihadarati aina ya bangi.

·
        
Kufanya mazoezi ili kuepuka unene uliozidi kipimo.

·
        
Kuepuka vilevi vikali.

·
        
Kuweka mazingira safi na salama kwa mwanadamu kuweza kuishi.

·
        
Kuepuka matumizi ya vyakula vyenye kemikali zenye sumu mfano; nyama nyekundu zilizosindikwa viwandani.

·
        
Kuepuka matumizi ya vipodozi vikali ili kujilinda dhidi ya saratani ya ngozi.

·
        
Kula vyakula vya asili ambavyo havitokani na mbolea za viwandani.
Zingatia
Si kila saratani inaweza kuzuilika kwa jitihada za binadamu bali ni baadhi tu kwani vyanzo vya ugonjwa huu ni vingi.  Mfano mzuri ni saratani ya kurithi ambazo ni vigumu kukwepeka kutokana na kurithiwa na wazazi.  Hata hivyo aina ya maisha anayoishi mtu na mazingira anayoishi huweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kuepukana na tatizo hili ingawa si kwa asilimia mia moja.  Mambo kama uchaguzi wa vyakula, vinywaji, kuepukana na matumizi ya sigara, ugoro na chumvi kwa wingi ni kati ya mambo yanayoweza kumsaidia mtu kuepukana na kansa za aina nyingi.

Soma pia TIBA ZA ASILI ZA UGONJWA WA SARATANI
Share:

No comments:

Post a Comment