Tuesday, February 21, 2017

IMARISHA KINGA ZA MWILI KWA KULA NANASI


nanasi huimarisha kinga ya mwili


Nanasi ni tunda linalopatikana kwa wingi nchini ingawa wengi hawafahamu umuhimu wake katika kuimarisha kinga za mwili, ili kujiweka mbali na maambukizi ya magonjwa kutokana na kupungua kwa kinga za mwili unashauriwa kula tunda hili kukabiliana na tatizo hilo.
Nanasi ni moja kati ya tunda lenye ladha nzuri mdomoni lakini lina vitamin nyingi na virutubisho vingi vyenye uwezo wa kuupa mwili nguvu na kuepuka kushambuliwa na maradhi.
Kwenye tunda hili kuna kirutubisho aina ya bromelain ambacho hulifanya nanasi kuwa muhimu katika kujenga na kuimarisha kinga ya mwili.
Ulaji wa mara kwa mara wa tunda hili husaidia kuimarisha kinga za mwili ambazo hukabiliana na kuvimba koo, ugonjwa wa baridi yabisi, ugonjwa wa gauti na hutibu matatizo ya tumbo ikiwapo bandama.
Wataalamu wa afya wanashauri ulaji wa tunda hilo kabla au baada ya kula mlo ili kuimarisha kinga za mwili dhidi ya maradhi mbalimbali.  Haishauriwi kula nanasi pamoja na chakula kingine kwa wakati mmoja.
Endapo hilo litafanywa, virutubisho vilivyopo katika nanasi vitafanya kazi nyingine tofauti na ile iliyokusudiwa.  Nanasi lina virutubisho vingi ikiwamo vitamin A, B na C na ina madini ya chuma, shaba na phosphorous ambayo ni muhimu katika afya ya binadamu.
Vilevile, tunda hili hutibu matatizo ya ini, homa, vidonda vya mdomoni, magonjwa ya koo na husaidia kusafisha utumbo mwembamba.
Kwa wale wanaopoteza kumbukumbu, nanasi lina uwezo wa kutibu tatizo hilo kwa watu wazima na vijana pia.
Mbali na faida hizo, nanasi lina uwezo wa kutibu kikohozi, kuondoa woga, kutetemeka na baridi yabisi.
Ulaji wa nanasi mara kwa mara husaidia kutibu maradhi ya akili, kukosa mori, kutibu matatizo ya wanawake hasa upungufu wa homoni na matatizo mengine ya sehemu za siri za mwanamke na husaidia kupata choo laini kwa wakati.
Tunda hilo husaidia kutibu upungufu wa damu na kuongeza maziwa kwa wanawake wanaonyonyesha.
Nanasi pia linajulikana kwa uwezo wa kuimarisha nuru ya macho.  Utafiti unaonesha ulaji wa tunda hili na mengine kwa kila mlo kwa siku kunaondoa hatari ya kupungua kwa nuru ya macho kwa asilimia 36 kwa watu wazima.
Share:

No comments:

Post a Comment