Monday, February 13, 2017

PUMU (Asthma)


Jopo la wataalam wa masuala ya afya nchini Marekani kipindi lilitoa takwimu kuhusiana na tatizo la ugonjwa wa pumu katika taifa hilo na duniani kwa ujumla.

Tafiti zinaonesha kuwa, Marekani ilikuwa na wagonjwa milioni 17 wa pumu tofauti na miaka mitano kabla kwani waathirika walikuwa milioni 14.5.

Pumu ni miongoni mwa magonjwa sugu ya hewa yanayosumbua idadi kubwa ya watu duniani na hasa watoto ambao wanakadiriwa kufikia zaidi milioni 5.5 huku idadi hiyo ikiongezeka siku hadi siku.

Lakini, pamoja na ukubwa wa tatizo hilo, bado kuna tumaini juu ya namna ya kukabiliana na ugonjwa huo kutokana na tafiti mbalimbali ambazo zinaendelea kufanywa na wataalamu wa masuala ya afya huku wakitoa suluhisho la kupunguza kikwazo hicho.

Uelewa wa Pumu

Pindi unapovuta pumzi, hewa huenda kwenye mdomo au pua kupitia katika mirija ya hewa na kusafiri hadi kwenye mapafu.  Katika mlolongo huu wa usafirishaji hewa kupitia mirija yake, tatizo la pumu huibuka pindi njia hizo zinapoingiliwa na kitu kutoka nje na kusababisha ugumu katika upumuaji.

Hali hii ya ugumu katika kupumua hujitokeza kutokana na kubana kwa mirija ya hewa kunakotokana na kubadilika kwa utendaji kazi wa viungo hivyo kunakotokana na kuchochewa na kitu kilichoingia kutokea nje iwe hewa chafu, vumbi au chavua ambacho huchochea kuundwa kwa sumu katika mwili wa mhusika huyo tu hata kama kitu hicho hakitakuwa na madhara kama hayo kwa mtu mwingine endapo kitaingia kwa njia ya hewa katika mirija yake ya hewa anapopumua.  Kitu hiki ndicho kijulikanacho kama Mzio au Aleji.

Kwa kiasi kikubwa tatizo la pumu hupatikana kwa njia ya kurithi na hasa kwa wale wenye matatizo ya mzio(aleji).

Aina za Pumu

Ugonjwa wa pumu umegawanyika katika makundi mawili huku kila moja likiwa na chanzo tofauti na lingine.

Aina ya kwanza ya ugonjwa huu hutokana na matatizo ya kurithi na hasa kwa wale watu wenye matatizo ya mzio (aleji), hivyo hufahamika kwa jina la allergic asthma ambavyo imesambaa sana kwenye nchi za Kiafrika ikiwemo Tanzania.

Aina hii ya pumu kwa kiasi kikubwa husababishwa na chavua(pollen), ukungu(Fog), wanyama, chembechembe za vumbi n.k.  Hata hivyo mizio mara nyingi hupatikana karibu kila sehemu.  Wakati chembechembe za vumbi na ukungu huingia kwa mwanadamu kupitia njia ya hewa, bado pumu ya mzio inaweza kuingia mwilini kupitia kitu chochote kilicholiwa mfano matunda aina ya strawberries.

Ukungu na vumbi lililo katika midoli pamoja na manyoya ya wanyama wa kufugwa wenye kupendeza ni hatari kwa mtu mwenye pumu kwani huchochea shambulizi la pumu ya mzio au Allergic asthma.

Aina ya pili ya ugonjwa wa pumu hufahamika kwa jina la (nonallrgic asthma), ambayo haitokani na matatizo ya mizio au kurithi kutoka kizazi kilichopita hivyo huweza kumkumba mtu yoyote kutokana na vyanzo vyake.  Ugonjwa huu husababishwa na hewa kavu, baridi kali, mazoezi, moshi, manukato yenye harufu kali, msongo wa mawazo na kadharika.


Uchafuzi wa mazingira na moshi utokanao na uvutaji wa sigara pia huchochea shambulizi la pumu.

Soma pia DALILI ZA UGONJWA WA PUMU
Share:

No comments:

Post a Comment