Monday, February 13, 2017

TIBA ZA ASILI ZA VIDONDA VYA TUMBO


TIBA YA MAJI

Tiba hii inafaa kwa kutibu vidonda vya tumbo vilivyo katika hatua za awali.

Mgonjwa anapaswa kunywa lita moja ya maji masafi na salama alfajiri kabla ya jua kuchomoza na kabla hajakisafisha kinywa chake wala kunawa uso au kupata kifungua kinywa.  Kisha mgonjwa anapaswa kusubiri kwa dakika 45 kabla ya kupata chakula cha mchana na asinywe maji yoyote baada ya kula chakula hicho cha mchana kwa dakika 45.

Wakati wa usiku mgonjwa anapaswa kunywa maji lita dakika 45 kabla ya kula chakula cha usiku na akae dakika 45 kabla ya kwenda kulala.

Tiba hii huchukua muda wa siku kumi mpaka mwezi mmoja kabla ya kupata nafuu.  Katika kipindi hiki chote mgonjwa anapaswa kuzingatia masharti juu ya ulaji na vitu vya kuepukwa.

Kabeji

Kunywa juisi ya kabeji mbichi baada ya kuikatakata  vipande kisha isage kwenye mashine ya kutengenezea juisi (Blender).  Baada ya hapo pima kwenye kikombe kimoja cha chai na unywe mara nne kwa siku.  Tiba hii inaweza kutibu tatizo la vidonda vya tumbo kwa muda wa siku kumi.  Kumbuka kuzingatia masharti ya msingi yaliyoainishwa hapo juu.

Asali

Asali ina chembechembe za asili zenye kuua bacteria na virusi ambazo vina uwezo wa kuua helicobacter Pylory ambao ni wadudu wanaosabisha ugonjwa huu kitu kinachomaanisha kuwa ina uwezo wa kutibu vidonda vya tumbo.  Kingine ni kwamba asali huweza kulainisha umio, mfuko wa chakula na utumbo hivyo huweza kufunika vidonda vilivyopo tumboni.  Kutokana na kufunika vidonda maumivu ya kuchoma pamoja na dalili nyingine za vidonda vya tumbo hupungua.

Asali pia huweza kusafisha uvimbe na kusafisha vidonda ambavyo hujitokeza kwenye njia ya chakula.  Asali inayopaswa kutumika kwa kusudio hili inapaswa iwe mbichi na isiwe imeongezewa vitu vingine na dozi yake ni vijiko vya chakula viwili mpaka vitatu kwa siku.

Vitunguu Swaumu

Viungo hivi ni tiba nyingine inayofaa sana katika kutibu vidonda vya tumbo kutokana na kemikali zinazoua wadudu pamoja na virusi zilizomo ndani yake na hivyo huweza kupambana na kuua bacteria wanaosababisha vidonda vya tumbo.

Viungo hivi hufahamika kwa kusaidia katika kutibu vidonda vya tumbo hata pale vinapotumika vikiwa vimechanganywa na vyakula vingine kutokana na nguvu nyingi iliyomo ndani yake pamoja na chembechembe zenye kuamsha na kuboresha mwili zilizomo ndani yake ambazo huwezesha kuukinga mwili dhidi ya maambukizi kama vile vidonda vya tumbo.

Hivi ndivyo unavyopaswa kutumia vitunguu swaumu kwa ajili ya kutibu tatizo hili:

Kula punje tatu mpaka nne za kiungo hicho kwa siku zikiwa zimechanganywa na kijiko kimoja au viwili vya asali kwa siku.

Jibini Ngumu Iliyosagwa (Grated Cheese)

Kula jibini ngumu husaidia kufunika vidonda vya tumbo hivyo hupunguza maumivu makali ya vidonda kwa hiyo iliwe kwa wingi na mtu mwenye tatizo hili na kwa wale ambao vidonda vyao vina muda mfupi tangu kujitokeza hupotea baada ya muda mrefu wa matumizi ya mara kwa mara ya chakula hiki.

Ukizingatia tiba hizi pamoja na masharti ya kufuata ukiwa unaugua ugonjwa huu yaliyoainishwa huko mwanzoni, kuna uwezekano mkubwa wa kupona tatizo hili na kuendelea kuishi maisha yenye furaha.
Share:

No comments:

Post a Comment