Wadau na mashirika mbalimbali yanayojihusisha na masuala ya
afya kote duniani huutumia mwezi huu kutathmini jitihada za kupambana na
saratani ya shingo ya uzazi, ugonjwa unaoongoza kuua wanawake wengi kuliko aina
nyingine yoyote ya saratani.
Hapo awali, wanawake walikuwa wanapoteza maisha baada ya
kupata maambukizi ya ugonjwa huu tofauti na hali ilivyo sasa kwani idadi ya
wanawake wanaopoteza maisha kutokana na saratani hiyo imepungua kutokana na
kampeni zilizofanyika kuongeza uelewa.
Wanawake hivi sasa hawana sababu ya kuendelea kupoteza
maisha kutokana na ugonjwa huu ingawa bado wanaendelea kufa. Saratani ya shingo ya kizazi bado inaendelea
kutishia maisha ya wanawake nchini.
Ripoti za karibuni zilizotolewa na Kituo cha Kudhibiti Magonjwa cha
Marekani (CDC) zinaarifu kuwepo kwa maelfu ya wanawake walio hatarini
kupatikana na saratani ya kizazi katika miaka michache ijayo huku sababu kubwa
ikiwa ni kukosa taarifa na uelewa wa kutosha.
Saratani ya shingo ya kizazi ni ugonjwa ambao huanzia na
kukua kwenye mlango wa uzazi maarufu kama cervix ambayo ni sehemu nyembamba
yenye uwazi inayoanzia ukeni hadi kwenye mfuko wa uzazi.
Saratani ya mfuko wa kizazi ndiyo inayoongoza kuua wanawake
wengi kuliko aina nyingine ya saratani ingawa ikigundulika mapema kunakuwa na
uwezekano mkubwa wa mgonjwa kupona.
Aidha, saratani ya shingo ya kizazi imethibitika kuwa ni
saratani inayozuilika kirahisi kuliko nyingine zote. Njia pekee ya kuzuia na kujikinga na saratani
hii ni kupata chanjo ya HPV; Human Pappiloma Viruses ambayo ni aina ya virusi
vinavyosababisha saratani hii.
Saratani hii huwashambulia wanawake pekee hivyo kumaanisha
hatari ya kwanza ni mwanamke mwenyewe.
Mara nyingi hutokea katika umri wa kati.
Zaidi ya nusu ya wanawake wanaopimwa na kukutwa na saratani hii huwa na
umri kuanzia miaka 30 hadi 60 ingawa huwapata pia wenye wastani wa miaka 20,
mara chache.
Inakadiriwa, asilimia 20 ya wanawake kuanzia miaka 60 na
kuendelea.
Sababu nyingine zinazomuweka mwanamke hatarini kupata
ugonjwa huu ni uvutaji wa sigara na aina yoyote ya tumbaku, maambukizi ya
ukimwi au magonjwa mengine ya ngono na hasa yanayojirudia, uzito uliopitiliza,
umasikini na sababu za kurithi zinazotokana na historia ya ugonjwa kwenye
familia.
Mwanamke wakati wote anashauriwa kuwa makini na dalili kuu
za ugonjwa huu kwani kupitia hizo zitampa msukumo wa kuwahi hospitali kuwaona
wahudumu wa afya na kupata vipimo ili kuiwahi saratani hii ikiwa kwenye hatua
za awali.
Dalili kuu za saratani ya shingo ya kizazi ambazo mwanamke
hapaswi kuzifumbia macho ni pamoja na kutokwa na damu kusikoendana na ratiba ya
mzunguko wake wa hedhi, kutokwa na damu wakati au baada ya tendo la ndoa au
wakati wa kujisafisha na hedhi isiyokoma kwa mwanamke ambaye hawezi kushika
mimba kutokana na umri.
Dalili nyingine ni ya mara kwa mara maumivu
chini ya kitovu, kutokwa na uchafu wenye rangi ya maziwa au njano unaoambatana
na harufu mbaya na maumivu wakati wa haja ndogo.
No comments:
Post a Comment