Friday, January 5, 2018

UTOAJI MIMBA KADHAA HAKUONDOI UWEZO WA KUZAA

utoaji mimba kadhaa

Hivi mtu aliyewahi kutoa mimba mara mbili na mpaka dakika hii bado hajapata ujauzito, je hapo baadaye akipata ujauzito ataweza kuzaa vizuri bila kupata shida yoyote? Na je atawahi au atachelewa kuzaa?

Kutoa mimba kinyume na sheria ni uondoaji wa kiumbe kilichotungwa kabla ya muda wa kuzaliwa haujafika pasipo sababu ya kitabibu.

Ieleweke kuwa si lazima utolewaji wa mimba kuwa na muingiliano wa uwezo wa mwanamke kupata mimba, jambo la msingi ni utoaji uwe ni salama na usio na madhara yoyote.

Katika nchi ambazo utoaji mimba si uvunjaji wa sheria, wanawake wengi hutolewa mimba na kuwa salama bila kujitokeza kwa madhara yoyote baadaye huweza kupata ujauzito mwingine wakiwa tayari kufanya kwa hilo.

Endapo mwanamke aliyetoa atajamiiana bila kinga yoyote anaweza kupata mimba nyingine ndani ya wiki mbili zitakazofuata baada ya yai lake la uzazi kupevuka.

Mtu anaweza kutoa mimba hata mara tano na akawa na uwezo wa kuzaa wakati wowote kama tu utoaji ulizingatia utaratibu unaotakiwa na hakuna madhara yoyote yaliyojitokeza.

Madhara yanayoweza kujitokeza kwa kutoa mimba ni pamoja na maambukizi ya via vya uzazi, majeraha ya mlango wa uzazi na ndani ya mfuko wa uzazi ndiyo yanayoweza kusababisha mtu kushindwa kupata ujauzito hapo baadaye au akipata inatoka.

Utoaji wa mimba kila mara bila ushauri wa daktari unaweza kusababisha majeraha katika mlango wa uzazi na kuufanya kuwa dhaifu na wakati wakubeba mimba zinaweza kutoka.

Maambukizi ya nyumba ya uzazi yanaweza yakatokea wakati au baada ya mimba kutolewa hivyo kutokea maambukizi kwenye via vya uzazi ikiwamo mirija kuharibika.

Kuwahi au kuchelewa kuzaa hili litategemea kama hakuna madhara yoyote yaliyojitokeza na mizunguko ya hedhi kurudi kama kawaida.

Inashauriwa kitaalam, mwanamke aliyetoa mimba au mimba yake kuharibika na kusafishwa apumzike kwa kipindi kati ya miezi 6 mpaka 12 au mwaka mzima kabla ya kushika ujauzito mwingine.

Kufanya hivi ni kuupa mwili nafasi ya kujijenga upya na homoni kurudi katika utaratibu wake wa awali.  Kumbuka, mimba inapotungwa kunatokea mabadiliko mengi mwilini ili kuandaa mazingira ya ukuaji wa mimba iliyotungwa.

Ni muhimu kuepukana na mimba zisizotarajiwa hasa kwa wasichana wanaosoma hii ni kutokana na changamoto zinazoweza kujitokeza ikiwamo kuachishwa masomo au kwenda zahanati za uchochoroni kutoa mimba hiyo.
Share:

2 comments:

  1. Kufanya hivi ni kuupa mwili nafasi ya kujijenga upya na homoni kurudi katika utaratibu wake wa https://photoshopcreative.co.uk/user/tuvanphathaionline kujitokeza ikiwamo kuachishwa masomo au kwenda zahanati za uchochoroni kutoa mimba hiyo

    ReplyDelete
  2. kujitokeza ikiwamo kuachishwa masomo au kwenda zahanati za uchochoroni kutoa mimba hiyo https://photoshopcreative.co.uk/user/tuvanphathaionline

    ReplyDelete